Uchafuzi wa hali ya hewa
Takwimu mpya za shirika la afya duniani (WHO) kuhusu ubora wa hewa, zimethibitisha kwamba asilimia 92% ya watu duniani wanaishi katika maeneo ambapo viwango vya ubora wa hewa ni vidogo kupita kiasi cha ukomo kilichowekwa na shirika hilo.
Takribani vifo milioni 3 kila mwaka vinahusishwa na hewa chafuzi hasa nje ya nyumba, lakini shirika hilo linasema hata ile ya ndani husababisha vifo pia.
Mwaka 2012 inakadiriwa kwamba vifo milioni 6.5 kote duniani vimetokana na hewa chafuzi ndani na nje ya nyumba huku karibu asilimia 90 ya vifo hivyo vikitokea katika nchi za kipato cha chini na wastani.