https://monetag.com/?ref_id=TTIb Barabara za TAMISEMi zaongezewa fedha hadi bil 247 | Muungwana BLOG

Barabara za TAMISEMi zaongezewa fedha hadi bil 247

Waziri wa nchi, ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. George Simbachawene mesema serikali imetenga shilingi bilioni 247.6 kwa mwaka wa fedha 2016/2017 kwa ajili ya ujenzi wa barabara zilizo chini ya TAMISEMI.

Amesema kiasi hicho ni mara 10 ya fedha ambazo zilikuwa zikitengwa awali ili kuboresha miundombinu ya barabara katika maeneo ambayo huzalisha malighafi mbalimbali zinazohitajika viwandani.

Mhe. Waziri Simbachawene ameyasema hayo kwenye mkutano watano kati ya TAMISEMI, Bodi ya Mfuko wa Barabara na wadau wa wakala wa Serikali za Mitaa.

Amesema kwa kutambua umuhimu wa barabara hizo serikali imeongeza fedha hizo kutoka shilingi Bilioni 23.8 za mwaka wa fedha 2015/2016 hadi shilingi Bilioni 247.6 kwa mwaka huu ili kuchochea ukuaji wa uchumi.

Aidha, amewaonya wakurugenzi wanaochelewesha kwa makusudi malipo kwa wakandarasi kuacha kufanya hivyo mara moja kwani vitendo hivyo vinachangia kuchelewesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kwamba mtu atakaye bainika atachukuliwa hatua za kisheria.