Samatta uwanjani leo kuiongoza Genk Vs Sasuolo

Mshambuliaji Mbwana Samatta, atakuwa na kazi wakati KRC Genk itakapokuwa inawavaa Waitaliano Sasuolo, kwenye mechi za makundi ya Ligi ya Europa.

Mechi hiyo ya Kundi F katika michuano ya Europa itakuwa ni hatua nyingine KRC Genk kujiweka vizuri katika michuano hiyo.

Samatta, alikosa michezo miwili iliyopita kwenye ligi kwa sababu ya majeruhi, lakini anarudi uwanjani kutaka kuisaidia klabu yake, iliyopoteza mchezo wa kwanza dhidi ya Rapid Wien.

Genk endapo itashinda mchezo wa leo, itajiweka mazingira mazuri kupigania kutinga 16 bora, katika kundi F.