Sifanyi kazi na meneja anayetafuta umaarufu - Nuh

Msanii Nuh Mziwanda ambaye hivi karibuni kulikuwa na tetesi za kuzinguana na uongozi wake akiwemo Petit Man ambaye anamsimamia, amesema ameamua kuachana kabisa na uongozi huo kwa mapenzi yake mwenyewe.

Nuh Mziwanda amesema ameamua kufanya hivyo kwani hana muda wa kupoteza tena, kwani meneja huyo anaonekana hana ujuzi wa kumsimamia.

"Nimetoka kule kwa ajili tu ya sababu zangu binafsi inabidi ni'move on, mi sio msanii mdogo inabidi niwe na meneja ambaye anajielewa na anajua msanii ambaye ninaye ni msanii ambaye yupo katika level gani, kama meneja anashindwa kujua msanii ambaye anafanya naye kazi siwezi kudeal naye, kwa sababu nilishapotezaga time katika muziki three years kwenye mapenzi, sa siwezi kupoteza mwezi mmoja kwa mtu ambaye kanikuta tu nimeamua kufanya naye kazi, kwa hiyo ni bullshit mi naachana naye naendelea na mambo yangu mengine", alisema Nuh mziwanda.

Nuh Mziwanda aliendelea...."Siyo kwa ubaya kwa uzuri, niliamua kufanya naye kazi, lakini kashindwa kupresent kile kitu ambacho mi nilikihitaji, narudia tena mi ni msanii mkubwa, inabidi ajue msanii mkubwa inabidi awe na nini na nini, kuna vitu avijue kama meneja, sasa kufanya kazi na meneja ambaye na yeye anataka ustar, ni kitu ambacho hakiwezekani", alisema Nuh Mziwanda.

Nuh Mziwanda pia alisema anaamini jitihada zake ndizo zimemfikisha hapo alipo, na kukanusha kauli ambayo watu wengi wamesema kuwa kwa kuwa sasa ana studio, amekuwa na dharau kwa uongozi wake.

"Naamini ndani ya jasho langu, nimehangaika nime'hustle' mpaka kufikia hapa, so kama watu wanaongea kuwa studio ndiyo imenifanya nigombane na meneja wangu si kweli, mi mtoto wa Kikristu, najua nafanya nini katika kazi yangu na napenda kulipa mazuri, sababu naamini ukimlipa mtu mazuri Mungu atakutendea mema katika maisha yako", alisema Nuh Mziwanda.