Taarifa za uzushi kuhusu kifo cha muigizaji Muhogo Mchungu.

 Kumeibuka  taarifa zisizo sahihi ambazo zimekuwa zikisambaa katika mitandao ya kijamii haswa Whatsapp na Instagram kuhusiana na muigizaji mkongwe wa filamu Tanzania, Muhogo Mchungu kufariki dunia. Baada ya taarifa hizo kuenea, kupitia mtandao wake wa Instagram, mwigizaji wa bongomovie Batuli amekanusha taarifa hizo.

Batuli aliandika hivi…

”Muogopeni Mungu Nyie Mnaozusha Habari Za Vifo Kwa Watu Maarufu,, Mkumbuke Hakuna Atakayepaa Sote Njia Yetu Ni Moja, Tumieni Mitandao Vizuri Sio Sifa Wala Ujanja Kutengeneza Habari Zenye Uzushi Kila Baada Ya Muda Fulani, Kifo Ni Cha Wote Hakikimbiliki Mtambue Ipo Siku Na Nyie Mabingwa Wa Kuzusha Kitawatembelea Tu #MunguAnawaona#MolaAkupeMaishaMarefuBaba”