Tasaf yawezesha miradi ya ufugaji

Bukombe. Baada ya kunufaika na fedha za ruzuku za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf), wakazi wa Kata ya Busonzo wilayani hapa Mkoa wa Geita, wameamua kuwekeza katika miradi ya ufugaji.

Mkazi wa Kijiji cha Nampalahala, Monica Mwombeki, amesema amekuwa akipokea Sh36,000 kila baada ya miezi miwili.

Amesema ameshapokea fedha hizo kwa awamu nane na zimemsaidia kufuga kuku hivyo kujiongezea kipato. Anatarajia kuwekeza katika ufugaji wa mbuzi, kondoo na kuku ili kuondokana na umaskini wa kipato.