Ujumbe kutoka CUF Tawi la UDSM

THE CIVIC UNITED FRONT (C.U.F - CHAMA CHA WANANCHI) JUMUIYA YA VIJANA (JUVICUF) C.U.F VYUO VIKUU TAWI LA CHUO KIKUU CHA DSM (UDSM-MLIMANI)

WITO KWA WANACUF
Chama cha wananchi C.U.F tawi la Chuo Kikuu UDSM kinapenda kuwajulisha wanacuf kuwa Ijumaa Septemba 30 wajumbe wa BARAZA KUU na WABUNGE wa C.U.F watawasili ofisi kuu za C.U.F taifa zilizopo BUGURUNI JIJINI DSM.

Katika msafara huo viongozi wakuu wa chama watakuwepo wakiwemo Katibu Mkuu taifa MAALIM SEIF SHARIFU AHMAD, mwenyekiti wa kamati ya uongozi CUF Mh JULIUS SUNDAY MTATIRO na viongozi wengine waandamizi wa chama.

Hivyo, Chama cha Wananchi CUF tawi la chuo kikuu cha DSM kinawaomba wanacuf wote kujitokeza kwa wingi mapema asubuhi kwenye ofisi hizo za BUGURUNI tayari kwa kufanya mapokezi makubwa ya viongozi hao wa chama ambao wanawasili ofisini hapo kwa lengo kuu la kupanga mikakati ya kukijenga chama.

Tunawaomba wanachama wote, vijana, wazee , akina mama, wanachuo wa CUF na wapenzi pamoja na wakereketwa wote wazalendo wa CUF kujitokeza kwa wingi wakiwa na vipeperushi vya chama, sare na kila aina ya vitu vyenye kuashiria upendo wa viongozi wetu wa CUF.

TUNAWAKARIBISHA WANACUF WOTE MAKAO MAKUU BUGURUNI KWA MAPOKEZI.

CUF ILIJENGWA NA WANACUF, IMEJENGWA NA WANACUF, INAJENGWA NA WANACUF NA ITAJENGWA NA WANACUF.

TUNAWATAKIA MAANDALIZI MEMA YA MAPOKEZI.

HAKI SAWA KWA WOTE

Imetolewa na :-
Mwl Razaq Mtele Malilo.
Katibu CUF vyuo vikuu tawi la Mlimani-UDSM.

Simu- +255625568417 / +255659913056

Barua pepe:  cufmlimani@gmail.com