Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad
Baadhi ya wafuasi hapo wamekusanyika eneo la ofisi hiyo wakiwa na nia ya kumpokea Profesa Lipumba na kumzuia Maalim Seif endapo atafika.
Akizungumza kwa niaba ya wenzake Juma Yassin amesema Maalim Seif ataendelea kubaki Zanzibar iwapo hatataka kumtambua Profesa Lipumba ambaye ni mwenyekiti halali Kikatiba.
"Tumesikia leo huenda akaja lakini ofisi na asijisumbue tupo tayari kwa lolote hadi amtambue Profesa Lipumba," amesema Yassin ambaye ni mwenyekiti wa Tawi la Kosovo Manzese.