Wasanii wa singeli tupunguze usela - Chokoraa

Mkali wa kurap na kuimba kutoka bendi ya Twanga Pepeta Khalid Chokoraa ameamua kuingia kwenye muziki wa kisingeli huku akiwataka wanamuziki wa kisingeli nchini kuacha kuuchukulia muziki huo kama ni wa kihuni.

Akipiga story ndani ya eNewz, Chokoraa amesema "Kikubwa zaidi nawasihi wasanii wa kisingeli kuangalia maneno wanayoyatumia na kupunguza maneno ya mtaani ili tuelimishe kupitia kisingeli".
Chokoraa alisema wasanii wa kisengeli ambao anatamani kuimba nao ni Sholo Mwamba, Man fongo na Makabila, na kwamba anatarajia kuachia video yake Jumatatu ya wiki hii na kuwataka mashabiki zake kuisubiri kwa hamu kwa kuwa wimbo huo unaelimisha, unaburudisha na una ujumbe mzuri kwa jamii.