Waziri wa Nchi, Ofisi Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), January Makamba amesema atazungumza na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais(Tamisemi), George Simbachawene kwa ajili ya kuajiri wataalamu wa mazingira wa mkoa huo.
Makamba amesema Sheria ya Mazingira ya mwaka 2004 inampa mamlaka waziri wa Tamisemi kuajiri au kuteua mtaalamu wa mazingira wa mkoa husika ambaye atakuwa kiungo kati ya mkurugenzi wa mazingira na baraza lake.
Waziri huyo amefikia uamuzi huo baada ya kupewa taarifa uongozi wa Songwe kuwa mkoa huo mpya hakuna mtaalamu wa mazingira, hali inayosababisha kushindwa kufanya shughuli zake kwa ufanisi.
Ofisa Mazingira wa Halmashauri ya Mbozi, Hamis Nzunda amesema endapo mtaalamu huyo akiajiriwa atakuwa msaada mkubwa mkoani humo.
Makamba amesema Sheria ya Mazingira ya mwaka 2004 inampa mamlaka waziri wa Tamisemi kuajiri au kuteua mtaalamu wa mazingira wa mkoa husika ambaye atakuwa kiungo kati ya mkurugenzi wa mazingira na baraza lake.
Waziri huyo amefikia uamuzi huo baada ya kupewa taarifa uongozi wa Songwe kuwa mkoa huo mpya hakuna mtaalamu wa mazingira, hali inayosababisha kushindwa kufanya shughuli zake kwa ufanisi.
Ofisa Mazingira wa Halmashauri ya Mbozi, Hamis Nzunda amesema endapo mtaalamu huyo akiajiriwa atakuwa msaada mkubwa mkoani humo.