Wafuasi wa Lema watinga mahakamani na fulana zenye ujumbe huu

Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema tayari amefikishwa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha kusikilizwa rufaa yake.


Mawakili wa pande zote walikutana kwa jaji kupeana taarifa  kabla ya kesi kuanza.

Ulinzi umeimarishwa mahakamani huku wafuasi wa Lema leo wametinga mahakamani na fulana nyeupe zimeandikwa Jutice 4 Lema mbele zikiwa na picha yake.