Picha: Vilio vyatawala wakati wa kuagwa wachezaji wa Chapecoense, Brazil

 Mji wa Brazil, nyumbani kwa timu ya Chapecoense iliyopoteza wachezaji wake kufuatia ajali ya ndege, ulikutana pamoja kutoa heshima zao za mwisho. Ndege iliyokuwa na wachezaji hao ilianguka Jumatatu hii nchini Colombia.
 Takriban watu 100,000 waliingia mtaani, nusu ya watu wanaoishi kwenye mji wa Chapeco na kuingia kwenye uwanja wa timu hiyo unaochukua watu 20,000. Mvua kubwa iliyonyesha, haikuwazua waombolezaji kushuhudia tukio hilo la kusikitisha.

Miili ya watu hao ilirudishwa kwao wakati ambapo imebainika kuwa rubani wa ndege hiyo, Miguel Quiroga raia wa Bolivia alizidanganya mamlaka za Colombia kuwa ndege ilikuwa na mafuta ya kutosha kuweza kumaliza safari. Ajali hiyo ilisababisha vifo vya watu 71.

Tazama picha zaidi: