Muda mchache Leo Oktoba 11, 2017 baada ya Aliyekuwa Waziri wa Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Angellah Kairuki kumkabidhi Ofisi Waziri George Mkuchika aliyeteuliwa hivi karibuni, Mkuchika amesema serikali imemaliza uhakiki na kubaini kuna watumishi elfu 40 walidanganya umri na hivyo wataondolewa ili wasibaki kwenye utumishi wa umma kwa muda ambao hawakustahili kuwa kazini.
TAZAMA FULL VIDEO HAPO CHINI