Rais
John Pombe Magufuli amefunguka na kusema kuwa kuanzia mwezi Novemba mwaka huu serikali ya awamu ya tano
itawapandisha vyeo na kurekebisha mishahara ya watumishi 59,967 baada
ya zoezi la uhakiki wa vyeti feki na hewa kukamilika
Rais
Magufuli amesema hayo leo kwenye sherehe za maazimisho ya mbio za
Mwenge wa Uhuru na kumbukumbu za miaka 18 ya kifo cha Baba wa Taifa
Mwalimu Nyerere sherehe ambazo zimefanyika visiwani Zanzibar. Rais
Magufuli katika hotuba hiyo alitolea mfano uzalendo wa Baba wa Taifa
ambaye aliamua kupunguza mshahara wake na kukata kuongeza mishahara ya
watumishi wachache huku walio wengi wakipata shida.
“Ninaposema
hivyo simaanishi kuwa mishahara isiongezwe. La hasha. Ninachosema ni
kwamba kabla ya kudai nyongeza ya mishahara ni lazima kwanza kufahamu
uwezo wa Serikali, lakini pia tutambue kuwa kuna Watanzania wenzetu
wengi tu wanaohitaji kuboreshewa huduma" Alisema
Rais Magufuli
TAZAMA FULL VIDEO HAPO CHINI