Waziri azindua mfumo wa Kieletroniki Utambuzi Wanamuziki

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe leo December 16, 2017   amezindua mfumo mpya wa Kieletroniki wa Utambuzi wa Wanamuziki ambao utaanza kutumika nchini kwa ajili ya kulinda maslahi ya wasanii.

Moja ya vitu ambavyo Dr. Mwakyembe amevizungumza ni kuhusu kuibiwa na kutumiwa kwa kazi za wasanii na watu wachache bila ridhaa yao  “tulipotoka ni kubaya, mimi nilikuwa DRC nilichoshangaa sana nilipita sehemu nikakuta picha kubwa ya Kanumba kule ni Star, ukija hapa mi nlifikiri kaacha mali za ajabu sana,”

“Vijana wetu wana  majina makubwa, mifukoni hawana kitu, mambo mengi yanaudhi ni kwenye sanaa, tutakwenda Mahakamani haiwezekani huu unyonyaji, ngoja tuondoe hii njaa ya mwanzo afu nianze kupambania mambo mengine,” – Dr. Mwakyembe