https://monetag.com/?ref_id=TTIb Taifa Stars kuwasili kesho | Muungwana BLOG

Taifa Stars kuwasili kesho

Kikosi cha Taifa Stars kimeondoka leo Algeria kupitia Dubai, ambapo kinataraji kuwasili nchini Tanzania kesho mchana.

Taifa Stars ilikuwa Algeria kwa ajili ya mchezo wa kirafiki ambao ni wa kalenda ya FIFA uliopigwa nchini humo kwenye Uwanja wa Julai 5.

Katika mchezo huo, Stars ilipoteza kwa jumla ya mabao 4-1 na kujiwekea mazingira magumu ya kupanda katika viwango vya ubora wa soka Duniani.

Stars itakuwa ina kibarua kingine cha mchezo wa kirafiki dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo utakaopigwa Machi 27 2018 jijini Dar es Salaam.