King Mswati abadilisha jina la nchi yake

Mfalme wa Swaziland, King Mswati III ametangaza kubadili jina la nchi hiyo na sasa itaitwa Kingdom of eSwatini ikimaanisha Ufalme wa eSwatini.

Mfalme huyo ametangaza mabadiliko ya jina hilo rasmi katika maadhimisho ya sherehe za miaka 50 ya Uhuru wa Swazi.

Sherehe hizo pia zimeadhimisha miaka 50 ya mtawala huyo ya kuzaliwa. Taifa hilo lililoko kusini mwa Afrika ni taifa lililo kwenye utawala kamili wa Kifalme.

Mfalme huyo anayejulikana kwa jina la Ngwenyama au “Simba”, anajulikana kwa kuwa na wake wengi na uvaaji wake wa kitamaduni.