https://monetag.com/?ref_id=TTIb Mabwawa mawili yakaribia kufurika nchini Kenya | Muungwana BLOG

Mabwawa mawili yakaribia kufurika nchini Kenya

Mabwawa mawili nchini Kenya yanakaribia kufurika kutokana na mvua kubwa , inayotishia maisha ya maelfu wa raia , kulingana na shirika la msalaba mwekundu lililozungumza na BBC.

Abbas Gullet , mkuu wa shirika la msalaba mwekundu nchini Kenya amewashauri raia wanaoishi katika eneo la Afrika mashariki na kati kuelekea katika maeneo ya juu.

Alisema kuwa takriban watu 200,000 wamewachwa bila makao kutokana na mafuriko huku wengi wakilazimikika kuishi katika shule ama maeneo yalio wazi.

Barabara zimejaa maji huku maporomoko yakiripotiwa katika maeneo mengine.

Mabwawa hayo ya Masinga na Kamburu hupata maji yake kutoka Mlima Kenya.

Watu wamekuwa wakisambaza picha katika mitandao ya kijamii kuhusu hatma ya mafuriko hayo, ikiwemo picha moja ya afisa wa msalaba mwekundu aliyekuwa akimsaidia mzee mmoja kusini mashariki mwa kaunti Tanariver , ambapo watu 50,000 wamelazimika kuyawacha makaazi yao.