Real Madrid yawasili Mjini Munich

Kikosi cha Real Madrid tayari kipo jijini Munich, Ujerumani tayari kuwavaa wenyeji wao Bayern Munich.

Wanakutana katika mechi ya kwanza ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, Madrid wakianzia ugenini.

Nyota wao, Cristiano Ronaldo yuko tayari kwa ajili ya mechi hiyo inayosubiriwa kwa hamu.

Hata hivyo, tayari Madrid imeonywa kwamba Bayern Munich si timu ya kudharau na wanapaswa kuwa makini sana hiyo kesho.