Nape Nnauye: Sitojali hatua yoyote serikali itakayochukua

Mbunge wa Jimbo la Mtama Nape Nnauye yupo Jimboni kwake ambapo kabla ya kushuhudia fainali ya Kombe la Dunia amezungumza na Wananchi wake juu mambo mbalimbali ikiwemo msimamo wake juu ya bei ya zao la Korosho.

“Duniani kazi ya Serikali ni kukusanya kodi, katika kupambana na umasikini wetu nilijua moja ya tatizo kubwa ni bei ya mazao yetu, wakazi wa Mtama ni wakulima na Mimi kwa kuwatetea wananchi sitojali hatua yoyote serikali itakayochukua” amesema Nape