Huu ndio ujumbe mzito alioutuma Zari kwa Daylan

Siku ya August 8 ilikuwa ni siku ya kuzaliwa mtoto wa Mwanamitindo Hamisa Mobetto aliyezaa na mwanamuziki Daimond Platinum aitwaye Daylan.

Katika siku hiyo ya kumbukumbu ya mtoto huyo ya kutimiza mwaka mmoja Daylan na Mama yake ambaye ni hamisa Mobetto walipata mwaliko katika ofisi za WCB ambapo waliungana na timu nzima ya WCB Aakiongozwa na Daimond mwenyewe amboa walimfanyia part ndogo kwa kukata keki na kumuimbia nyimbo za Birthday.

Siku ya jana zari alifanyiwa interview na kituo cha runinga cha NBS cha uganda akaulizwa anaichukuliaje siku ya kuzaliwa ya mtoto Daylan na hivi ndivyo alivyojibu;

"Happy birthday Daylan! naamini utapata yaliyobora maishani na Aunt Zee anakupenda  vyovyote vile umma utasema  halikuwa kosa lako ulijikuta tu katika hili na ndomana ukatokea internet siku zote itakusema kuwa ni mtoto uliyekuja kubomoa nyumba nyingine mtoto aliyezaliwa kutokana na kosa vyovyote watakavyosema kama hupo hapa naamini utakuja kuwa kitu bora" alisema Zari

Ikumbukwe kuwa Daimond amezaa watoto wawili na Zari na Mtoto mmoja kutoka kwa Hamisa Mobetto kwa hiki alichikionyesha zari naamini Daimond amekifurahia kwakuwa siku ya birthday ya mama yake alitoa ushauri kwa wazazi wenzake kuwa kila mtu ampende mtoto wa kila mmoja kwakuwa ni ndugu na malezi hayo yatasaidia kuwaunganisha watoto hao katika shida na raha pale watakapokuwa wakubwa.