Shonza asifu ubunifu unaoneshwa na wasanii nchini


Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza amesema wizara yake iko bega kwa bega na wasanii wa filamu ikiwemo kulinda haki zao na kuongeza kuwa haitamuacha pekee msanii yeyote anayehitaji msaaada wa kiserikali kwa kuwa fani hiyo imewapatia ajira vijana wengi hapa nchini.

Shonza ameyasema hayo wakati akizindua filamu ya Nipe Changu yake msanii Duma katika ukumbi wa Mlimani City ambapo aliwasifu wandaaji wa filamu hiyo kutokana na ubora wa kazi yao lakini pia ubunifu ambao wameutumia katika kuandaa.

Pia aliwataka wasanii hao kufanya kazi zao kiumakini ili kuwa na ubora wa kimataifa na kujizolea soko ndani na nje ya nchi ili wapate kunufaika na kipato.