Wakizungumza baada ya kumuokoa mhandisi huyo, asubuhi ya leo tarehe 22 Septemba 2018, baadhi ya waokoaji walisema mbinu ya Mhandisi Charahani ya kujipaka oil mwilini, ilimsaidia kuzuia maji ya ziwa hilo kuingia kwenye vinyweleo vyake.
Kivuko hicho kilizama kwenye ajali iliyotokea tarehe 20 Septemba 2018 wakati kikisafirisha abiria kutoka kisiwa cha Bugorora kwenda Kisiwa cha Ukara kwenye Ziwa Victoria.
Baada ya kuokolewa, Mhandisi Charahani alikimbizwa katika Kituo cha Afya cha Busya kilichopo kisiwani Ukerewe kwa matibabu zaidi.