Simba SC bila Masoud Djuma yashindwa kuibuka na ushindi tena


Kwa mara ya kwanza klabu ya Mbao imefanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Simba kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

Mchezo huo wa Ligi Kuu Bara umemalizika kwa bao pekee kufungwa na Said Hamis mnamo dakika ya 26 kwa njia ya penati baada ya kipa Aishi Manula kumdondosha straika wa Mbao, Pastory Athanas kwenye eneo la hatari.

Matokeo hayo yanaifanya Simba kusalia na alama zake 7 huku Mbao ikifika kileleni kwa kujikusanyia pointi 10.

Aidha, mechi nyingine mbili za Ligi Kuu Bara zilipigwa leo ambapo Kagera Sugar ikiwa ugenini Mbeya imelazimisha sare ya mabao 2-2 dhidi ya Tanzania Prisons.

Singida United waliokuwa Uwanja wa Uhuru kucheza na African Lyon wamepokea kichapo cha mabao 3-2.