SMZ inatambua mchango wa Wanadiaspora katika kuleta maendeleo Nchini

 Na.Thabit Madai,Zanzibar.

Serikali ya Mapinduzi ya zanzibar imesema inatambua na kuthamini jitihada zinazofanywa na wanadiaspora katika kuchangia, kukuza na kuimarisha sekta mbali mbali za maendeleo nchini ikiwemo sekta ya Afya.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Issa Haji Ussi pamoja na  Waziri wa Afya Hamad Rashid Mohammed jana  Ikulu mjini Zanzibar wakati walipofanya mazungumzo na Timu ya Madaktari Wazalendo waishio Marekani kutoka Taasisi ya Afya, Elimu na Maendeleo (Head Inc).

Waziri Gavu alisema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inathamini sana mchango wa Wanadiaspora hao ambao wameonesha uzalendo wa hali ya juu katika kutoa huduma za afya kwa kuwahudumia wananchi waliotoka katika maeneo kadhaa ya hapa Zanzibar.

Pia waziri Gavu alitoa pongezi kwa Timu hiyo kwa uwamuzi wake wa kuja Zanzibar kwa lengo la kutoa huduma za afya kazi ambayo wameifanya kwa ufanisi na mafanikio makubwa.

Katika maelezo yake, Waziri Gavu alisisitiza kuwa huduma zilizotolewa na Timu hiyo yenye makao makuu yake nchini Marekani zimeweza kusaidia kwa kiasi kikubwa ambapo wananchi walio wengi walipata fursa ya kuangalia afya zao na kupata tiba.

Aliongeza kuwa juhudi zaidi zinaendelea kuchukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha huduma za afya ikiwa ni pamoja na kuimarishwa kwa miundombinu ya sekta hiyo, vifaatiba, rasilimali watu na mambo mengineyo.

Mapema Waziri wa Afya Hamad Rashid Mohamed alieleza kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendeleza ushirikiano wake na Wanadiaspora hao kutoka Taasisi hiyo ambao wamejitolea kuwasaidia ndugu zao na kulisaidia Taifa lao.

Alieleza kuwa ni faraja kubwa kwa kufikiwa na Madaktari hao ambao miongoni mwao wamo Madaktari Bingwa wa maradhi mbali mbali ambao walipata fursa ya kutoa huduma za afya kwa wananchi waliotoka maeneo mbalimbali katika mikoa ya Kusini na Kaskazini Unguja ambapo walitumia Hospitali ya Makunduchi na Hospitali ya Kivunge kama ni vituo kwa ajili ya kutoa huduma za afya kwa wananchi.
 Katika maelezo yake, Waziri Gavu alisisitiza kuwa huduma zilizotolewa na Timu hiyo yenye makao makuu yake nchini Marekani zimeweza kusaidia kwa kiasi kikubwa ambapo wananchi walio wengi walipata fursa ya kuangalia afya zao na kupata tiba.

Aliongeza kuwa juhudi zaidi zinaendelea kuchukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha huduma za afya ikiwa ni pamoja na kuimarishwa kwa miundombinu ya sekta hiyo, vifaatiba, rasilimali watu na mambo mengineyo.

Mapema Waziri wa Afya Hamad Rashid Mohamed alieleza kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendeleza ushirikiano wake na Wanadiaspora hao kutoka Taasisi hiyo ambao wamejitolea kuwasaidia ndugu zao na kulisaidia Taifa lao.

Alieleza kuwa ni faraja kubwa kwa kufikiwa na Madaktari hao ambao miongoni mwao wamo Madaktari Bingwa wa maradhi mbali mbali ambao walipata fursa ya kutoa huduma za afya kwa wananchi waliotoka maeneo mbalimbali katika mikoa ya Kusini na Kaskazini Unguja ambapo walitumia Hospitali ya Makunduchi na Hospitali ya Kivunge kama ni vituo kwa ajili ya kutoa huduma za afya kwa wananchi.

Katika maelezo yake, Waziri Hamad alieleza juhudi zilizochukuliwa na zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha sekta ya afya Unguja na Pemba.

Alitumia fursa hiyo kueleza mikakati iliyowekwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuhakikisha huduma za afya zinaendelea kutolewa bure kama ilivyoelekezwa na Serikali hatua ambayo imeweza kuwasaidia wananchi walio wengi wakiwemo wasiokuwa na uwezo.

Aidha, Waziri Hamad alieleza hatua zinazoendelea kuchukuliwa katika kutatua changamoto kadhaa katika sekta hiyo huku akisisitiza kuwa elimu ya afya kwa wananchi itaendelea kutolewa ili kufikia lengo lililokusudiwa.

Nao Madaktari kutoka Taasisi hiyo walipata fursa kueleza jinsi walivyotoa huduma za afya zikiwemo tiba pamoja na elimu ya afya kwa wananchi katika hospitali walizofika huku wakipongeza jinsi mapokezi makubwa waliyoyapata hatua ambayo imepelekea kufanya shughuli zao za kutoa huduma za afya kwa ufanisi mkubwa.
Sambamba na hayo, Madaktari hao walizipongeza juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inazozichukua katika kupambana na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI ambapo walieleza katika huduma zao zote walizozitoa hakupatikana hata mwananchi mmoja aliepata maambukizi.

Pia, Madaktari hao walipongeza hatua za Serikali katika kupamabana na maradhi ya Malaria ambapo Zanzibar imepata mafanikio makubwa ikilinganishwa na nchi nyingi za Bara la Afrika huku wakiahidi kutoa vifaa tiba kwa wananchi wa Zanzibar.


Madaktari hao pia, walisisitiza haja ya kuchukua tahadhari zaidi kutokana na  kuwepo kwa ongezeko la maradhi yasiokuwa ya kuambukiza hasa shinikizo la damu na kisukari hiyo ni kutokana na wananchi waliowengi kuonekana kuwa na dalili za maradhi hayo baada ya uchunguzi waliofanya.


Pamoja na hayo, Madaktari hao walieleza haja ya kuendelea kutolewa elimu ya afya kwa wananchi wa Zanzibar hasa wanaoishi vijijini. Katika Taasisi hiyo pia, wamo Madaktari kutoka nchini Lesotho ambao walishirikiana pamoja na Wanadiaspora.