Messi avunjika kiungio cha mfupa wa mkono


Mshambuliaji wa timu ya Barcelona Lionel Messi ameumia mkono katika mchezo wa La Liga dhidi ya Sevilla ambapo alinza akiwa mzima kabisa.

Baada ya kufanyiwa Vipimo kutokana na majeraha aliyoyapata, imebainishwa kuwa staa wa Barcelona, Messi amevunjika kiungio cha mfupa wa mkono wake wa kulia, Hivyo atakaa nje kwa wiki tatu akiuguza jeraha hilo huku akiukosa mchezo wa wapinzani wao Real Madrid Oktoba 28 mwezi huu.

Katika mchezo huo Barcelona walishinda bao 4-2.