https://monetag.com/?ref_id=TTIb Faida za kula uyoga | Muungwana BLOG

Faida za kula uyoga

1. Uyoga ni chanzo kikubwa na kizuri cha vitamin C, D na Potassium.
2. Uyoga unaondoa hatari ya kuwa na kansa kwa kupambana na kuviondoa vianzilishi vya kansa za aina zote.
3. Uyoga ni tiba ya kisukari kwa waliothariwa tayari na ambao hawajaathiriwa huwa ni kinga pia.
4. Uyoga hufanya damu kuwa nyepesi na hivyo kurahisisha mzunguko wake mwilini na hivyo kuondokana na uchovu na maumivu ya viungo.
5. Uyoga huondoa lehemu iliyoko kwenye moyo hivyo kupambana na Presha ya damu.
6. Uyoga hutibu magonjwa ya athma kwa kuweka mfumo wa upumuaji vyema na hutibu mzio (allergies)
7. Uyoga hutibu na kuzuia matatizo ya figo.
8. Uyoga huimarisha mfumo wa fahamu.
9. Uyoga hupambana na virus visababishavyo HIV/AIDS, hivyo hupunguza makali yake kwa kiwango kikubwa.

JE UNA SABABU GANI YA KUKOSA KULA UYOGA WEWE NA FAMILIA YAKO

NB: Wataalam wanashauri kula uyoga angalau mara mbili kwa wiki kutokana na manufaa yake kiafya.

Onana na wakulima wa uyoga na ununue uyoga uliolimwa kitaalamu kwa bei ya shilingi kati ya 7,000/ na 10,000/ tu kwa kilo moja (inategemea na ulipo), uyoga uliolimwa kitaalam huwa hauna madhara yoyote kwani hupandwa mbegu maalum isiyo na sumu wala madhara katika mwili wa binadamu.

Kikubwa, epuka kununua uyoga wa porini ambao utashindwa kutambua upi ni sumu na upi siyo sumu na hivyo kuhatarisha maisha yako na ya familia yako.

Epuka uyoga wa kwenye makopo una kemikali za kuuhifadhi na hivyo kupunguza ubora wake, tafuta uyoga fresh kutoka kwa wakulima​