Mradi kabambe wa teknolojia ambao utajumuisha makampuni tofauti ya teknolojia wataraji kuanza mjini Kigali katika eneo la hekari 70.
Mradi huo utaanikishwa nchini Rwanda kwa ushirikiano na jukwaa la maendeleo ya miundombinu la benki ya maendeleo ya Afrika .
Jukwaa hilo linafahamika kama ”Africa 50”.
Mradi huo utatumia kiwango cha dola bilioni 2 huku Benki ya Maendeleo ya Afrika ikifahamisha kwamba itatumia kiwango cha dola milioni 400.
Mradi huo unajumuisha ujenzi wa vyuo vikuu, vituo vya teknolojia ya kisasa na vituo vya biashara.
Wanafunzi zaidi ya 2600 kila mwaka watakuwa wakihitimu katika mafunzo ya teknolojia.
Waziri mkuu wa Rwanda Edouard Ngitente amesema kuwa mradi huo ni miongoni mwa miradi ya ”Vision 2020” ambao ni malengo ya Rwanda kufikia ifikapo mwaka 2020.