Watu 42 wafariki na wengine wajeruhiwa baada ya basi walilokuwemo kulipuka moto jana usiku Gwanda nchini Zimbabwe.
Msemaji wa jeshi la Polisi la usalama barabarani Gwanda amesema kuwa watu 42 ndio ambao wamefariki katika ajali hiyo ya moto iliotokea katika basi la abiria usiku wa Alkhamis.
Kulingana na taarifa zilizotolewa muda mchache baada ya ajali, moto huo huenda ulisabishwa na mtungi wa gesi uliolipuka.
Shirika la msalaba mwekundu la Zimbabwe limerusha katika ukurasa wake wa Twitter picha ya ajali hiyo zikionesha basi hilo lilivyoteketea kwa moto.