https://monetag.com/?ref_id=TTIb Beno Kakolanya atimuliwa Yanga | Muungwana BLOG

Beno Kakolanya atimuliwa Yanga

Mwinyi Zahera

Kocha wa Yanga Mwinyi Zahera amesema hawezi tena kufanya kazi na mlinda mlango Beno Kakolanya kwasababu sio mzalendo kwa timu.

Mwinyi Zahera ameweka wazi hilo jana usiku baada ya Beno kurejea kambini kwa mara ya kwanza tangu alipotoka kwenye kambi ya timu ya taifa iliyocheza na Lesotho Novemba 18, 2018.

''Nawaambia viongozi huyu mtu wamtafutie timu kabla ya dirisha la usajili kufungwa, simtaki tena ndani ya Yanga, timu zipo nyingi aende akacheze huko kwa waliokuwa wamemzuia kuja mazoezini'', alieleza Zahera.

Zahera amesisitiza kuwa anafahamu wakala wa mchezaji huyo ni miongoni mwa viongozi wa Simba hivyo hawezi kufanya naye kazi baada ya kupotea kwa muda mrefu sasa hana imani naye.

''Mtu hayupo na sisi kwa muda bila sababu maalum na tulimtafuta akawa hasemi chochote sasa kwa taarifa zilizopo ni kwamba mtu anayefanya naye kazi ni kiongozi wa Simba, na kama atarudi akakaa langoni kuachia magoli itakuwaje, yeye aende tu'', aliongeza Zahera.

Yanga ipo kambini ikijiandaa na mchezo wake wa kesho jumapili dhidi ya Ruvu Shooting  utakaopigwa kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es salaa.