Leo Disemba 12 Rais wa Chama Cha Madaktari Tanzania, Dkt. Elisha Osati ameiomba Serikali kuhakikisha wanatatua changamoto za wahudumu wa afya nchini ili waweze kufanya kazi kiuweledi.
Dkt. Osati ametoa kauli hiyo siku chache tu mara baada ya Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Jerry Muro kufanya ziara ya kustukiza
usiku wa manane katika hospitali mbili Za Wilaya kujionea hali ya utoaji
wa huduma za Afya nyakati za usiku.