Morgan Heritage na Patoranking wafanya video Maasai Mara


kundi la Muziki wa Reggae kutoka nchini Jamaica, Morgan Heritage wamefanya video kwenye Mbuga ya Wanyama maarufu nchini Kenya, Maasai Mara.

Kundi hilo limeeleza video hiyo ni kwa ajili ya wimbo utakaofuata kuutoa wakiwa wamemshirikisha Patoranking kutoka nchini Nigeria.



"Just arrived in the Maasai Mara for day 3 of the video shoot for our next single," wameeleza Morgan Heritage kupitia ukurasa wao wa Instagram.

Utakumbuka kuwa Morgan Heritage walijipatia umaarufu zaidi nchi mara baada ya kushirikishwa na Diamond Platnumz kwenye wimbo wake unaokwenda kwa jina la Hallelujah uliotoka September 2017.