https://monetag.com/?ref_id=TTIb Ruby amhoji Shetta 'Unataka kushindana na Diamond Platnumz?, Kisa? | Muungwana BLOG

Ruby amhoji Shetta 'Unataka kushindana na Diamond Platnumz?, Kisa?



Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva,  amefunguka ishu iliyopelekea yeye kuondoka lebo King Empire ambapo walikuwa pamoja na Shetta.

Ruby kuwa msanii huyo mwenzake alikuwa ni mtu wa  fitna kwa Bosi wao  huku akimhoji kuwa alikuwa anataka awe kiongozi yaani ana lebo kama Diamond Platnumz mwenye lebo ya WCB.

"We fikiria mpaka Shetta anakwambia aah! tutamtoa huyo hatujui sisi kama wazee wa fitna maana yake atamtoa katika cheo chake cha u general ina maana atamtoa kupitia Boss, ataenda kumfanyia fitna kwa Boss . Lakini wewe Shetta unataka kuniambia una nguvu gani kwa Boss mtu General Meneja atolewe pale eti uwekwe wewe msanii ambaye huna hata lebo unataka ushindane na Diamond ambaye yeye ana Wasafi WCB alafu uonekane una King Empire," amesema Ruby.

Shetta ambaye ni mmoja kati ya viongozi wa labo ya King Empire ambayo inawasimamia wasanii kama Aslay, The Mafik na wengine.