Na. Rahel Nyabali, Tabora.
Wanafunzi zaidi ya 16,000 ambao wanaingia kidato cha kwanza mwaka huu mkoani Tabora wanakabiliwa na upungufu wa vyumba vya madarasa zaidi ya 250.
Ilikuweza kukizi ongezeko la huku asilimia sabini na tano ya wanafunzi elfu kumi na moja watoro sugu na rejareja waliojaribu kuacha masomo wamerejea tena shuleni na hivyo ongezeko hilo limesababisha kuwepo kwa upungufu mkubwa wa vyumba vya madarasa.
Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa huu, Agrey Mwanri katika Kikao kinachowakutanisha viongozi wa Serikali na viongozi wa Chama cha Walimu (CWT) Mkoa wa Tabora kikiwa na malengo ya kujadili hali ya maboresho ya Elimu kwa shule za Msingi na Sekondari,Suala la upungufu wa Vyumba vya Madarasa linapewa kipaumbele.
Hata hivyo, Suala la nidhamu ya walimu na wanafunzi,pamoja na chakula shuleni ni mambo mengine yaliyochukua nafasi katika majadiliano ndani ya kikao hicho ikiwa ni lengo la kuinua sekta ya Elim.
Aidha CWT Mkoa wa Tabora kimeihakikishia Serikali kushilikiana nayo katika kutekeleza wajibu na majukumu waliopewa walimu maeneo yao ya kazi huku ikilipa ikienda kinyume na suala la migomo ambayo lilikuwa likijitokeza hapo awali wakati wa kudai haki stahili za walimu kwa mwajiri.