Wahamiaji wawasili mpakani mwa Marekani na Mexico

Wahamiaji kutoka katika baadhi ya mataifa ya Amerika Kusini wameanza kuwasili  mpakani mwa Marekani na Mexico huku wengine wakiripotiwa kuomba hifadhi mpakani mwa Guatemala na Mexico, baada ya kuomba hifadhi   wahamiaji hao huendelea na safari yao ambayo malengo yao ni kuingia nchini Marekani.

Uongozi wa shirika la kutetea haki za wahamiaji  INM  umeomba kuondolewa na vikosi vya usalama kwa lengo  la kuzuia kutokea  ghasia baina yao na  wahamiaji.

Mexico imeongeza idadi ya maafisa wa idara  ya uahamiaji katika mpaka wake wa Kusini kwa lengo la kuzuia msongamano wa mwahamiaji mpakani. Taarifa ziznafahamisha kwamba wahamiaji wanaoingia Mexico kutoka Amerika Kusini watapewa hifadhi katika kambi  ya  Suchiate.

Idara ya uhamiaji ya Guatemala  amefahamisha kuwa raia takriban 700 kutoka Honduras na  107 kutoka El Salvador  wamevuka mpaka wakiwa  katika safari yao kuelekea nchini Marekani.