Indonesia yakumbwa na tetemeko la ardhi

Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 5.2 limetokea katika eneo la Maluku kaskazin mwa Indonesia.

Kwa mujibu wa habari,tetemeko hilo limefikia kina cha kilomita 44.1.

Hakuna mtu aliyeripotiwa kupoteza maisha au mali kuharibika na hakujatolewa tangazo lolote la kutahadhari kuwepo kwa uwezekano wa kutokea kwa Tsunami baada ya tetemeko hilo.

Watu wengi hupoteza maisha kutokana na matetemeko y aardhi ambayo yamekuwa yakitokea mara kwa mara nchini Indonesia.