Magaidi 15 wa Al Shabab wauawa katika mashambulizi ya anga ya jeshi la Marekani

Magaidi 15 wa Al Shabab wauawa katika mashambulizi ya anga ya jeshi la Marekani nchini Somalia.

Kwa mujibu wa habari,mashambulizi hayo ambayo yalifanyika ndani ya masaa 48 yamepelekea vifo vya magaidi hao katika mkoa wa Shebelle.

Shambulizi la kwanza lilifanyika 6 mwezi Februari huko Gendershe, na kuua wanamgambo 11, wakati shambulizi la pili likiwa limefanyika Februari 7 huko Bariire na kuua  wapiganaji wanne.

Kulingana na taarifa nchini Somalia,shambulizi la Bariire limefanyika baada ya jeshi la Somalia kushambuliwa na wanamgambo wa kundi hilo la kigaidi la Al Shabab.

Mashambulizi hayo ya  anga yamekuwa yakifanyika siku ya nne sasa.