Meddie Kagere: Sina habari na kazi za kwenye mitandao ya kijamii


Mshambuliaji wa Simba SC,  Meddie Kagere amefunguka kuwa hana mpango wa kujitamba kwenye mitandao ya kijamii badala yake ataonyesha kazi kubwa uwanjani.

Kagere ameendeleza makali yake Ligi Kuu Bara kwa kufunga mabao mawili kwenye mechi mbili mfululizo akianza ule wa Mwadui FC na mchezo wa watani wa jadi Yanga Uwanja wa Taifa kwa kufunga bao la ushindi dakika ya 71.

"Sina habari na kazi za kwenye mitandao ya kijamii kazi yangu mimi uwanjani, huku ndiko hasira zangu zilipo, yale ambayo yamepita kwangu ni historia nafanya mipango mingine," amesema Kagere.

Kagere anafikisha mabao tisa kwenye msimamo wa wafungaji huku kinara akiwa na Herieter Makambo wa Yanga mwenye mabao 11.