Serikali yamaliza sakata la makontena yaliyokwama Bandarini Dar


Serikali imetatua kadhia ya makontena ya wafanyabiashara wa DRC kukwama Bandarini, Dar es Salaam na sasa makontena hayo yameanza kutoka Bandarini.

Waziri Kamwelwe amesema makontena hayo yalizuiwa baada ya kujitokeza tena tuhuma za baadhi ya wa wafanyabiashara kubakiza nchini bidhaa zilizopaswa kwenda nje ya nchi.
Kaimu Balozi wa DRC nchini naye amemshukuru Rais Magufuli na Waziri Kamwelwe kwa kulimaliza tatizo lililojitokeza katika taratibu za forodha na ameahidi atasimamia wafanyabiashara wa DRC kufuata sheria za nchi.