Simba yatakiwa kufuta uteja kwa vilabu vya Congo kesho


Katika michezo 34 Simba waliocheza wakiwa kama wenyeji tokea 1976 ni vilabu 11 tu vimefanikiwa kuondoka na alama.

1977: Simba 0-0 Kwara
1978: Simba 0-1 AS Vita
1980: Simba 2-4 Union Duala
1995: Simba 1-1 Powerd Dynamos
1995: Simba 1-2 Assec Mimosas
2003: Simba 0-0 Santos
2003: Simba 0-0 Ismailia
2005: Simba 1-1 Enyimba
2008: Simba 1-3 Enyimba
2011: Simba 2-3 Tp Mazembe
2013: Simba 0-1 Libolo

Vilabu viwili vya Congo TP mazembe na AS Vita hawajahi kufungwa hapa Tanzania. Ni wajibu wa Simba kufuta uteja huo hapo kesho.

Kama tunavyoona hapo historia ya Simba wakiwa nyumbani imejitahidi sana kuhakikisha heshima ya taifa hili inalindwa. Simba imepoteza mechi 5 lakini imeshinda michezo 22. Rekodi ya mechi 4 za mwisho Simba imepata matokeo chanya kwa kushinda zote.