https://monetag.com/?ref_id=TTIb Baby wangu sio tajiri, tutafunga ndoa kawaida - Lulu | Muungwana BLOG

Baby wangu sio tajiri, tutafunga ndoa kawaida - Lulu


Msanii wa Filamu Bongo, Elizabeth Michael 'Lulu' amesema kuwa yeye na Mchumba wake, Majizo ni watu wa kawaida hivyo watafunga ndoa ya kawaida.

Lulu amesema kuwa kutakuwa na watu wa upande wa kike na wa kiume na baadhi ya marafiki zao.

“Mimi na mwenza wangu Majizzo bado hatujaoana. Sisi tabia zetu zinaendana ni watu wa kawaida hivyo tutafunga ndoa kawaida yaani ndugu upande wa kiume na upande wa kike pamoja na marafiki zetu baadhi," Lulu ameiambia Clouds FM.

"Baby wangu sio tajiri bali ni mtu ambaye ameanzia chini kimaisha mpaka kufika alipofika na am proud kwa hilo.”