Kocha wa Serengeti Boys akiri kuwa golikipa ni changamoto


Baada ya kupoteza mchezo wa jana wa michuano ya mataifa ya Afrika kwa vijana chini ya miaka 17 dhidi ya Nigeria kwa kufungwa goli 5-4,Kocha mkuu wa timu ya Taifa ya vijana 'Serengeti boys' Oscar Mirambo amekiri kuwa katika nafasi ya Golikipa kuna changamoto katika kikosi chake.

" Changamoto kweli ipo kwa Golikipa lakini tunapompa nafasi tena anazidi kuimarika na kujua kuwa alikosea wapi katika mchezo uliopita " Mirambo

Mirambo aliongeza kuwa japo wamepoteza mchezo wa jana lakini bado Serengeti boys ina nafasi ya kufanya vizuri kwa michezo miwili iliyobaki.

Pia alisisitiza kuwa muda huu sio wa kuwalaumu vijana kwa kutofanya vizuri , sasa ni wakati wa kuwaweka sawa ili waweze kufanya vizuri katika michezo iliyobaki.

"Tunachotakiwa kufanya kwa sasa ni kuweza kuwaweka sawa watoto ili wasahau yaliyopita na kujiandaa na mechi zilizobaki" Mirambo

Tanzania atakuwa Mgeni wa Uganda katika mchezo unaofuata utakaochezwa April 17 mwaka huu saa 11.00 jioni kwenye Uwanja wa Taifa na mechi ya mwisho watacheza na Angola April 20.