Mkuu wa Mkoa, Wilaya atakae msweka mtu mahabusu bila sababu kuchukuliwa hatua


Waziri wa Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, George Mkuchika amesema kuwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya wenye tabia ya kuwasweka mahabusu watu wasiokuwa na hatia watachukuliwa hatua.

Mkuchika amesema kuwa mtu nawekwa ndani kama ana hatarisha amani sio watu wanadaiana madeni huko una muweka ndani, mtu asiwekwe mpaka awe amehatarisha amani.

“Mkuu wa mkoa au mkuu wa wilaya wanapotumia Mamlaka yao ya kuweka mtu mahabusu kwa saa 48 na 28 wazingatie sheria ya Tawala za Mikoa, " amesema Mkuchika Bungeni jijini Dodoma.

"Akitekeleza sheria kinyume na utaratibu kinyume na utaratibu anaweza kuchukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na yeye mwenyewe kushitakiwa binafsi, Mwanasheria mkuu wa Serikali hatomtetea mtu aliyevunja sheria makusudi kwa kumuweka mtu ndani bila sababu."