Lowassa na mkewe waibuka Ujerumani


Waziri mkuu Mstaafu Edward Lowassa akiwa na mkewe Mama Regina Lowassa nchini Ujerumani. Mhe Lowassa yuko nchini Ujerumani kwa shughuli zake mbalimbali.

Hata hivyo bado haijaelezwa kitu gani kilichompelea kiongozi huyo wa zamani nchini humo hadi kufikia sasa.

Lowassa hajaonekana hadharani kwa kipindi kirefu tangu alipotangaza uamuzi wake wa kurejea Chama cha Mapinduzi (CCM) akitokea Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kilichompa dhamani ya kugombea Urais mwaka 2015.