Ijue nchi inayotajwa kuwa na usalama zaidi duniani


Iceland imetajwa kuwa ndiyo nchi salama zaidi duniani ikishikilia nafasi hiyo kwa mara ya 11 mfululizo.

Kwa kuzingatia vigezo 23 ikiwa ni pamoja na migogoro ya ndani na nje ya nchi hiyo, matumizi ya kijeshi, ugaidi,mauaji na viwango vya uhalifu wa aina nyingine.

Nchi 17 za Ulaya ziko katika nafasi ya juu kati ya nchi 25 zenye amani zaidi duniani kwa mujibu wa utafiti. Aidha zaidi ya watu milioni 400 duniani wanaishi katika maeneo yenye usalama mdogo na hatari kubwa ya mabadiliko ya tabia nchi.