Rais wa zamani wa Gambia afilisiwa mali zake zote na serikali


Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Waziri wa Sheria ya Gambia, Abubacarr Tambadou hapo jana  katika mkutano na waandishi wa habari alisema kuwa mali zote za Rais wa zamani wa nchi hiyo, Yahya Jammeh zimetaifishwa na serikali.

Tambadou aliongeza kuwa ofisi yake inachukua hatua zote za kumshauri Rais juu ya ripoti hiyo, na kuongeza kwamba mali za Jammeh zilizobinafsishwa na serikali zinajumuisha mali zote zilizozalishwa kwa sasa ambazo tayari zipo.