Singida United yasaka wachezaji 25, wajitokeza 200 kwenye usahili


Wachezaji zaidi ya 200 kutoka mikoa mbalimbali nchini wamejitokeza katika majaribio ya kusaka nafasi ya kuichezea Singida United yaliyoanza jana kwenye Uwanja wa Namfua mjini Singida.

Kocha Peter Magomba ambaye amepewa jukumu la kusaili wachezaji hao amesema ni wachezaji 25 pekee ndiyo wanaotakiwa kutoka kwenye majaribio hayo ya siku tano.