Timu ya Alliance FC yamsubiri kocha wao kujua hatma

Uongozi wa timu ya Alliance FC umesema kuwa kwa sasa wanamsubiri kocha wao Malale Hamsini asaini kandarasi mpya ili aendelee na kazi kwani msimu uliopita alifanya mambo makubwa.

Kwa sasa Hamsini amemaliza mkataba wake na bado hajasaini mkataba mpya kwa kile alichodai kwamba bado hajawasiliana na viongozi wa Alliance FC.

Akizungumza na Salehe Jembe, Ofisa Habari wa Alliance, Jacson Mwafulango amesema kuwa wanaamini uwezo wa Hamsini hali iliyofanya wamuandalie mkataba mapema.

"Sisi Alliance tunatambua kwamba Hamsini ni kocha wetu ndio mana tumemuandalia mkataba hivyo kilichobaki kwa sasa ni yeye mwenyewe kusaini ili kuendeleza mipango kwa ajili ya msimu ujao," amesema.