Dhoruba kali ya upepo yaua watu 6 na wengine 108 wajeruhiwa

Watu 6 wameripotiwa kufariki na wengine 108 wamejeruhiwa miongoni mwao wanne wamejeruhiwa vikali kutokana na dhoruba kali iliotokea nchini Ugiriki.

Kituo cha runinga cha taifa cha ERT  kimesema kuwa  upepo mkali umekumba eneo la  Kaskazini, eneo ambalo ni kivutio kwa watalii.