Wasiokuwa na vyeti halali vya kuishi Marekani kuondolewa, Maandamo yaibuka


Maelfu ya waandamanaji nchini Marekani wamepinga operesheni ya Marekani iliyotangazwa na Rais Donald Trump ya kuwakamata na kuwaondoa wahamiaji na familia zao wasiokuwa na vyeti halali vya kuishi nchini humo.

Operesheni hiyo iliyopangwa kuanza wikiendi hii itapelekea maafisa wa kitengo cha udhibiti wa wahamiaji, ICE, kuingia katika mitaa ya miji karibu 10, kuwakamata watu karibu 2,000.